1 Chronicles 16:23-28


23 aMwimbieni Bwana dunia yote;
tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.

24 bTangazeni utukufu wake katikati ya mataifa,
matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.

25 cKwa kuwa Bwana ni mkuu,
mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote;
yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.

26 dKwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu,
lakini Bwana aliziumba mbingu.

27 Fahari na enzi viko mbele yake;
nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.

28 eMpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa,
mpeni Bwana utukufu na nguvu,
Copyright information for SwhKC